Wakaja na kanzu yake ina damu ya uwongo. Akasema: Bali nafsi zenu zimekushawishini kutenda kitendo. Lakini subira ni njema; na Mwenyezi Mungu ndiye wa kuombwa msaada kwa haya mnayo yaeleza.
–Sura Yusuf [12:18]
فصبر جميل عسى الله ان ياتيني بهم جميعا انه هو العليم الحكيم ٨٣
Akasema: Bali nafsi zenu zimekushawishini kwenye jambo fulani. Subira ni njema! Asaa Mwenyezi Mungu akaniletea wote pamoja. Hakika Yeye ni Mjuzi Mwenye hikima.
–Sura Yusuf [12:83]
انما اشكو بثي وحزني الى الله واعلم من الله ما لا تعلمون ٨٦